Skip to main content
Nukta the Podcast

Nukta the Podcast

By Nukta Habari

Nukta Habari inakusogeza na mambo mtambuka yanayokuhusu ikiwemo burudani, mtindo maisha, safari, teknolojia na biashara.
Available on
Google Podcasts Logo
Pocket Casts Logo
RadioPublic Logo
Spotify Logo
Currently playing episode

From sunlight to harvest: How solar energy brings hopes to farmers in Iringa

Nukta the PodcastMar 17, 2024

00:00
07:52
From sunlight to harvest: How solar energy brings hopes to farmers in Iringa

From sunlight to harvest: How solar energy brings hopes to farmers in Iringa

For decades, farmers in Lupembe Lwa Senga village in Iringa region had relied on the traditional farming system for their livelihoods. Apart from using hand hoes, animal plows, they would wait for the rain to irrigate their crops.  

For small plots like gardens, they would use buckets or recently fuel-powered water pumps for irrigation. 

“We started irrigation farming as a group in1999, by that time we were using a fuel-powered pump with the cost of 200,000 for buying petrol to irrigate all five acres a day, it was terrible,” Gabriel Mmewa, farmer in Lupembe Lwa Senga said. .

With outdated oil pump machines driving the irrigation process, he said the cost of production soared, leaving the farmers trapped in a cycle of diminishing returns.

However, as the demands of a growing population and the uncertainties of rains, the need for innovation became apparent.

Mar 17, 202407:52
UPUNGUFU WA WALIMU SHULE YA MSINGI UNAVYOATHIRI ELIMU TANZANIA
Sep 30, 202309:35
Elimu ya Veta inavyowainua walemavu wa akili Tanzania

Elimu ya Veta inavyowainua walemavu wa akili Tanzania

Awali, ilikuwa ni vigumu kushuhudia watu wanaozaliwa na ulemavu wakipata huduma muhimu wanazozihitaji kama elimu, afya, pamoja na kushirikiana na wanajamii wengine kuibua suluhu za matatizo yanayozikabili jamii zao.

Hivi sasa zama hizo zimepita. Kutokana na hatua zilizochukuliwa na Serikali pamoja na wadau, ikiwemo kuielimisha jamii kutowabagua na kushirikiana na kundi hilo, kama binadamu wengine watu wenye ulemavu nao wanapata huduma wanazostahili.

Miongoni mwao ni kijana Paulo Ngunyali, mhitimu wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kilichopo Chang’ombe, Jijini Dar es Salaam. Pamoja kuwa mlemavu wa akili amehitimu fani ya uundaji wa mashine, na sasa ni mwalimu msaidizi katika kitengo cha watu wenye mahitaji maalumu.

Katika maonesho ya kimataifa ya kibiashara maarufu kama Saba Saba, Paulo (32), amekuwa kivutio cha wengi kutokana na namna anavyoelezea kwa ufasaha jinsi mashine ya kupima uwezo wa kufundishaa  watu wenye ulemavu wa akili inavyofanya kazi.

Sep 15, 202308:00
MFAHAMU MBUNIFU WA MAJIKO YANAYOTUMIA MAWE TANZANIA

MFAHAMU MBUNIFU WA MAJIKO YANAYOTUMIA MAWE TANZANIA

Nishati ya kupikia ni miongoni mwa mahitaji muhimu ya binadamu duniani kote, hiyo ndio huwezesha mapishi ya aina mbalimbali za vyakula tunavyokula ili kuimarisha afya na kuwezesha utendaji wa shughuli za kila siku.

Watu wengi wanatambua gesi, mkaa, umeme, mafuta pamoja na kuni kama ndio vyanzo vya nishati ya kupikia kwa kuwa ndio ambavyo vinatumika kwa kiasi kikubwa kwa sasa huku jitihada nyingi zikielekezwa kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Hata hivyo, jijini Dar es Salaam kuna ubunifu mpya wa nishati ya kupikia inayotumia mawe, ambapo inatajwa kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za kupikia kwa gesi, umeme, mkaa au nishati nyingine.

Ndiyo! Ubunifu, udadisi pamoja na uthubutu umewezesha ugunduzi huu ambapo sasa mawe yanayopatikana kwa urahisi katika maeneo mengi nchini Tanzania yanaweza kutumika kama chanzo cha nishati ya kupikia.

Raymond James (25) maarufu kama Mr Majiko, ndiye mbunifu wa majiko hayo yanayotumia mawe, umeme kidogo pamoja na chenga za mkaa mbadala zinazotokana na vifuu vya nazi.

Kijana huyo mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, ameiambia Nukta Habari kuwa kukosa ajira ndio sababu kubwa iliyommchochea kubuni majiko hayo ili aweze kujiingizia kipato kitakachomuwezesha kuendesha maisha.

Katika podcast hii, amezungumza mengi. karibu kumsikiliza

Sep 08, 202307:42
JINSI MATAPELI WANAVYOTUMIA TAASISI YA MO FOUNDATION KUIBIA WATU

JINSI MATAPELI WANAVYOTUMIA TAASISI YA MO FOUNDATION KUIBIA WATU

 Kama wewe ni mtumiaji wa mtandao wa Facebook huenda umewahi kukutana na chapisho linalohusu fursa ya mikopo kutoka kwenye taasisi ya mfanyabiashara bilionea nchini Tanzania Mohamed Dewji Foundation

Sehemu ya chapisho hilo lianasomeka ‘𝐉𝐈𝐏𝐀𝐓𝐈𝐄 𝐌𝐊𝐎𝐏𝐎 𝐊𝐔𝐓𝐎𝐊𝐀 𝐌𝐎𝐇𝐀𝐌𝐄𝐃 𝐃𝐄𝐖𝐉𝐈 𝐅𝐎𝐔𝐍𝐃𝐀𝐓𝐈𝐎𝐍 kwa maelekezo ya kupata vigezo na masharti njoo hwatspp kwa no👉🏿 0748923136’.

Chapisho hilo pamoja na kuhamasisha watu kuomba mikopo wametaja kigezo cha kutoa kwanza kiasi cha hisa ya mkopo unaotaka kupewa kabla ya kupata mkopo wenyewe.

Ufafanuzi zaidi wa taarifa hiyo unaonesha kama unahitaji kukopa Sh100,000 basi utalazimika kutoa kwanza hisa ya Sh22,000 ndipo upewe mkopo huo.

Taarifa hiyo imesambaa katika mtandao wa Facebook kupitia akaunti zenye majina tofauti tofauti toka mwaka 2022  huku ikiwa imeambatanishwa na  video fupi inayomnukuu Mohamed Dewji kuwa anatoa mikopo.

Hata hivyo, Habari hiyo haina ukweli wowote kwa kuwa ni habari za uzushi zinazotumiwa na matapeli kuwalaghai wananchi na kujipatia vipato kwa njia zisizo halali. 

Nukta Fakti imefanya utafiti ili kubaini ukweli wa akaunti hizo za mtandao wa Facebook na kugundua kuwa akaunti hizo hazina uhusiano wowote na Mohamed Dewji mwenyewe au taasisi yake ya Mohamed Dewji Foundation.

Akaunti sahihi ya Facebook ya mfanyabiashara huyo maarufu nchini ni Mohammed Dewji huku ile ya taasisi yake ni Mo Dewji Foundation na sio Mikopo Tanzania kama inavyojitambulisha akaunti hiyo inayodai kutoa mikopo.

Mohamed Dewji hatoi mikopo

Utafiti zaidi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa, si Mohamed Dewji mwenyewe wala taasisi yake ambayo inajihusisha na utoaji wa mikopo kwa namna yoyote ile.

Kupitia mtandao wa Linkedin Mohamed Dewji amewahi kutoa taarifa kwa umma akifafanua kuwa taasisi yake inajihusisha zaidi kutoa misaada ya kielimu kwa kufadhili masomo, upatikanaji wa maji pamoja na kutatua changamoto katika sekta ya afya.

Sep 01, 202307:30
KWA NINI BANGI INALIMWA ZAIDI TANZANIA LICHA YA OPARESHENI KALI ZA DAWA ZA KULEVYA?

KWA NINI BANGI INALIMWA ZAIDI TANZANIA LICHA YA OPARESHENI KALI ZA DAWA ZA KULEVYA?

Mapema Agosti mwaka huu Serikali ya Tanzania ilitangaza kukamata magunia 131 ya bangi, kilo 120 za mbegu za bangi na kuteketeza jumla ya hekari 489 za mashamba ya bangi mkoani Morogoro, katika moja ya operesheni kubwa za kutokomeza dawa za kulevya iliyowahi kufanyika nchini. 

Katika operesheni hiyo Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Aretas Lyimo anasema wakulima hao wa bangi hufanya uharibifu mkubwa wa mazingira kwa kuchepusha maji pamoja na kukata misitu ili kufanya kilimo cha zao hilo haramu.

Watu 18 walikamatwa katika operesheni hiyo iliyoshika mjadala katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii baada ya mamlaka hiyo kueleza kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakifanya kilimo katika mazingira ambayo si rahisi kufikika. 

Hili ni miongoni mwa matukio makubwa ya kudhibiti dawa za kulevya ndani ya miaka mitano, jambo linaloashiria kuwa washirika wa dawa hizo hatari kwa afya ya binadamu wanaendelea kuzalisha licha ya jitihada za Serikali na wadau kuzidhibiti.

Mwaka 2021 tani 22.74 za bangi zilikamatwa nchini Tanzania ikiwa ni ongezeko la asilimia 72 ya kiasi kilichokamatwa mwaka 2020.

Aidha, takwimu za uhalifu nchini zilizopo katika kitabu cha hali ya uchumi mwaka 2022 kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonesha mashamba ya bangi yameongezeka takriban mara mbili ndani ya miaka minne kutoka 49 mwaka 2018 hadi kufikia mashamba 87 mwaka 2022.

Aug 25, 202309:13
Teknolojia ya vifuu vya nazi itakavyo waokoa wachimbaji na madhara ya zebaki
Aug 18, 202307:07
Hizi ndio hifadhi tano kubwa za Taifa, Tanzania

Hizi ndio hifadhi tano kubwa za Taifa, Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa mataifa ambayo yamebarikiwa vivutio vingi vya utalii ambavyo sio tu vinapendezesha nchi bali ni chanzo kizuri cha mapato hususani fedha za kigeni ambazo hutumika kwa shughuli za maendeleo.

Tovuti ya runinga ya Tanzania Safari Channel ambayo hutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini, inabainisha kuwa Asilimia 40 ya ardhi ya Tanzania imetengwa kwa ajili ya uhifadhi.

Hii inajumuisha hifadhi za Taifa 22, eneo la hifadhi ya Ngorongoro, mapori tengefu, hifadhi za misitu asilia na misitu ya kupandwa, maeneo ya kihistoria pamoja na hifadhi za bahari.

Maeneo yote hayo ndio kitovu kikubwa cha utalii nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa kitabu cha hali ya uchumi kwa mwaka 2022, kinachotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) hifadhi za taifa ni moja kati ya vivutio vilivyotembelewa zaidi na watalii wa ndani na nje ya nchi.

Mwaka 2022 hifadhi hizo zilitembelewa na jumla ya watalii milioni 1.4 kati yao watalii 787,742 walitoka ndani ya nchi na watalii 697,264 kutoka mataifa mengine yaliyopo nje ya  nchi.

Huenda wewe ni miongoni mwa watu wanaofahamu kuhusu uwepo wa hifadhi hizi lakini hujui ni ipi inaongoza kwa ukubwa, inapatikana wapi, na gharama za kufika huko.

Makala hii imeorodhesha hifadhi tano ambazo ndio kubwa zaidi nchini Tanzania pamoja na aina ya vivutio utakavyokutana navyo.

Aug 11, 202307:11
MVUVI MPAMBANAJI NDANI YA ZIWA VICTORIA

MVUVI MPAMBANAJI NDANI YA ZIWA VICTORIA

Ziwa Victoria ni moja ya maziwa makuu ya Afrika Mashariki. Ni ziwa ambalo lipo kwenye mstari wa ikweta na limezungukwa na nchi tatu zilizopo Afrika Mashariki yaani Tanzania, Kenya na Uganda.

Ziwa hili ni chanzo cha Mto Nile wenye urefu wa kilomita 6,650 na urefu huo unaufanya kuwa mto mrefu zaidi duniani, Ziwa Victoria ndiyo ziwa kubwa zaidi barani Afrika na lina ukubwa wa kilomita za mraba 68,800 ambapo ni la pili duniani kwa ukubwa likitanguliwa na Ziwa Superior lililopo Amerika ya kaskazini, kwa ukubwa huu nchi za Rwanda na Burundi zinaweza kuwa visiwa ndani ya ziwa hili.

Ziwa hili linahudumia wakazi takribani milioni 40 wa Afrika Mashariki kupitia shughuli za uvuvi, utalii na usafirishaji ambazo hufanyika kila siku, miongoni mwa wanaotegemea ziwa hili katika shughuli zao za kila siku ni Mwajuma Chamuriho, mwanamama huyu amejiajiri na ametengeneza ajira zaidi ya 50 owa watu wengine kupitiz Ziwa Victoria.

lakini Mwajuma ni nani hasa, nini kilimsukuma kuwekeza katika uvuvi kazi ambayo inatafsiriwa kuwa nya wanaume zaidi, fuatana na Abdulshakur katika makala hii ya dakika saba, natumai utajifunza mengi.

Mar 21, 202306:18
ELIMU YA SAIKOLOJIA INAVYOWABEBA WATU WENYE UALBINO TANZANIA

ELIMU YA SAIKOLOJIA INAVYOWABEBA WATU WENYE UALBINO TANZANIA

Watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Tanzania wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali unyanyapaa ikiwa miongoni, licha ya afua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali kuelimisha watu wanaowazunguka, baadhi ya walemavu hushindwa kujumuika na wanajamii wengine kutokana na hofu au mitizamo ya kifikra waliyonayo wao wenyewe hata kama jamii ina mtizamo chanya juu yao.

Abdushakur Mrisho ametuandalia makala yanayoonesha ni kwa namna gani elimu ya saikolojia inavyoweza kuwakomboa watu hawa na kuwafanya wajione kama watu wengine na kuchangamana na wanajamii wengine katika shughuli za kijamii.


Mar 21, 202309:15
Ifahamu zahanati iliyoanzishwa kwa mkopo wa halmashauri

Ifahamu zahanati iliyoanzishwa kwa mkopo wa halmashauri

Ni Zahanati ya Afya ya Jamii iliyopo Kata ya Kipunguni jijini Dar es Salaam ambayo ni ya kwanza katika kata hiyo. Vijana nane wametumia mkopo Sh100 milioni wa Halmashauri ya Ilala kuianzisha ili kupunguza changamoto za afya jijini humo. Esau Ng'umbi anasimulia zaidi.

Oct 01, 202208:20
Mradi wa umemejua unavyowafaidisha wanavijiji Tanzania

Mradi wa umemejua unavyowafaidisha wanavijiji Tanzania

Ni mradi wa jiko linalotumia mionzi ya umemejua kupikia vyakula mbalimbali. jiko hilo la aina yake limebuniwa na Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. 

Jun 03, 202207:30
Wazazi wanavyopambana kuwapatia chakula wanafunzi shuleni Pangani

Wazazi wanavyopambana kuwapatia chakula wanafunzi shuleni Pangani

Salaaam msikilizaji wa NUKTA THE PODCAST karibu katika muendelezo wa makala zetu na leo tunasafiri hadi Wilayani pangani mkoani Tanga kumulika namna wazazi wanavyopambana kuwapatia chakula wanafunzi katika shule za sekondari, i mimi ni Suleman Omar Mwiru.

Apr 22, 202206:35
Zaidi ya Watanzania 500,000 kukumbukwa na uhaba wa chakula

Zaidi ya Watanzania 500,000 kukumbukwa na uhaba wa chakula

Wakati baadhi ya Watanzania wakila na kusaza kiasi cha kutupa chakula, ripoti mpya ya usalama wa chakula na lishe Tanzania inakadiria kuwa kuanzia Mei 2022 watu 592,000 watakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na kushuka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo nchini.

Ripoti hiyo ya Tathmini ya Usalama wa Chakula na Lishe iliyotolewa Februari 2022 na Wizara ya Kilimo na Idara ya Udhibiti Maafa ya Ofisi ya Waziri Mkuu imeeleza kuwa hali hiyo ya uhaba mkubwa wa chakula itashudiwa kati ya mwezi Mei hadi Septemba mwaka huu.

Nini sababu? Herimina Mkude anasimulia zaidi.

Mar 25, 202203:30
“Show” ya kibabe iliyowakutanisha mastaa wa Afrika

“Show” ya kibabe iliyowakutanisha mastaa wa Afrika

‘Young, Famous & African’ au kwa kifupi unaweza kuita YFA, ni ‘reality show’ yaani imebeba uhalisia wa maisha ya wahusika.

Natumaini katika pita pita zako kwenye mitandao ya kijamii, umeshakutana na jina hilo.

Wahusika wake ni vijana nyota, maarufu na wenye ‘mishiko’ yao haswaa kutoka nchi mbalimbali Afrika.

Ndani humo utakutana na ‘Dj’ maarufu kusini mwa Afrika, hapa namzungumzia Dj Naked, muimbaji Nadia, mtangazaji maarufu Afrika Kusini Andile, nyota wa muziki kutoka Nigeria 2baba na wengineo.

Bila kuwasahau Zari na Diamond, ambao tunaweza sema wamesababisha Watanzania wengi kuitazama show hiyo.

Mar 25, 202205:49
Jukumu la kutunza mazingira ni la kila mtu

Jukumu la kutunza mazingira ni la kila mtu

Utunzaji wa mazingira yanayotuzunguka ni njia mojawapo ya kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi ikiwemo mafuriko na ongezeko la joto. 

Mar 25, 202201:41
 Ukame ulivyowarudisha wafugaji kwenye umaskini Tanzania

Ukame ulivyowarudisha wafugaji kwenye umaskini Tanzania

Mwaka 2021 unavyoanza alikuwa ana matumaini lukuki kuwa ng’ombe wake aliokuwa nao wangechangia kwa kiwango kikubwa kumuongezea kipato na kumtoa katika umaskini.

Miezi 11 baadaye ndoto ya Ndirana Ndirana Jijungu, mkazi wa Kijiji cha Mwamihanza wilayani Maswa mkoani Simiyu ilizimwa ghafla kwa kupoteza ng’ombe wanne kati ya sita baada ya kukosa malisho kutokana na ukame. Hata hivyo, ukame wa mwishoni wa mwaka 2021 umemfanya apoteze sehemu kubwa ya mali na kumrudisha kwenye umaskini.

Tofauti na miaka mingine, mvua hizo zilichelewa kiasi cha kuathiri upatikanaji wa malisho na maji maeneo mengi wilayani Maswa, kama anavyosimulia Herimina Mkude.

Mar 24, 202206:00
Mbinu zitakazosaidia kudhibiti taka za baharini

Mbinu zitakazosaidia kudhibiti taka za baharini

Kudhibiti uchafuzi wa bahari Serikali na wadau wanasema taasisi za utafiti na viwanda zinahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano ikiwemo kuimarisha mifumo ya ulejerezaji taka. Pia kupiga marufuku kabisa matumizi ya chupa za plastiki na kutoa elimu kwa wananchi juu ya uhifadhi wa mazingira ya bahari kama anavyoripoti Suleman Mwiru. 

Mar 23, 202205:53
Gharama kubwa zinavyorudisha nyuma jitihada za kuokoa mazingira Wilaya ya Kibaha

Gharama kubwa zinavyorudisha nyuma jitihada za kuokoa mazingira Wilaya ya Kibaha

Baada ya kubaini faida na urahisi wa kutumia nishati ya gesi kupikia, mwalimu wa moja ya shule za sekondari wilayani Kibaha aliamua kuchukua hatua.

Alianza jitihada za kutumia gesi kuongeza ufanisi katika mapishi shuleni kwao na kupunguza kiasi cha kuni zinazotumika kupikia ili kuokoa mazingira. Hata hivyo, changamoto iliyobaki ni gharama kubwa za kupata nishati hiyo. Herimina Mkude anatujuza zaidi.

Mar 22, 202205:48
Changamoto zinapokuletea fursa

Changamoto zinapokuletea fursa

Ni filamu ya "Fine Wine", inayomuhusu mwanadada Kaima anayepitia changamoto katika mahusiano. Licha ya uzuri na ‘usmati’ alionao binti huyu, mahusiano yake na kijana Tunji ni pasua kichwa kuliko hata majukumu yake ya kazi.

Maisha ya Kaima yanabadilika siku ambayo wanakubaliana kukutana na Tunji katika mgahawa fulani, lakini kaka huyo anamwambia mpenziwe kuwa amsubiri kwani kuna jambo la ghafla limetokea.

Mar 18, 202207:55
Taka za kielektroniki zinavyotafuna mazingira ya Tanzania

Taka za kielektroniki zinavyotafuna mazingira ya Tanzania

Hakuna mifumo mizuri ya kutupa taka za kielektroniki nchini Tanzania kama ilivyo kwenye nchi zilizoendelea hivyo suluhu kubwa iliyopo ni kuzitupa kama taka nyingine.

Mar 14, 202204:21
The Last Royal Treasure: Filamu ya kuchangamsha wikiendi yako

The Last Royal Treasure: Filamu ya kuchangamsha wikiendi yako

Filamu ya ‘The Last Royal Treasure’, inahusu kundi moja la maharamia au kwa Kiingereza wanafahamika kama pirates.

Meli yao imebeba watu ambao wana historia tofauti za kimaisha. Wengine walikuwa majenerali wa vita, watoto wa manahodha, huku wengine wakiwa ni wezi walioshindikana.

Mar 11, 202206:48
Changamoto zinazorudisha nyuma urejelezaji taka Tanzania

Changamoto zinazorudisha nyuma urejelezaji taka Tanzania

Ukosefu wa elimu ya udhibiti wa taka hasa plastiki, sera na sheria zinazosimamia mazingira zimetajwa na wadau wa mazingira kuwa zinaweza zikachelewesha safari ya kupunguza uharibifu wa mazingira hasa unaosababishwa na taka za plastiki. 

Mar 10, 202207:02
Chupa za plastiki za vinywaji vya kuongeza nguvu zinavyochocheo uharibifu wa mazingira

Chupa za plastiki za vinywaji vya kuongeza nguvu zinavyochocheo uharibifu wa mazingira

Kuzagaa kwa chupa za plastiki za rangi zinazotumika kuhifadhia vinywaji vya kuongeza nguvu katika mitaa mbalimbali nchini Tanzania hasa jijini Dar es Salaam kumeibua changamoto mpya ya kudhibiti uchafuzi wa mazingira.

Licha ya chupa za maji kuokotwa kwa ajili ya kufanyiwa urejelezaji, chupa za rangi zimekuwa zikiachwa zikizagaa mitaani kwa sababu wenye viwanda hawazihitaji katika shughuli zao. 

Nini kinafanyika kudhibiti taka hizo? Herimina Mkude anaeleza kwa undani suala hilo.


Mar 05, 202207:01
Magugu maji yanavyowatesa watumiaji wa Ziwa Victoria

Magugu maji yanavyowatesa watumiaji wa Ziwa Victoria

Kuendelea kuwepo kwa magugu maji katika Ziwa Victoria kumeibua kadhia mbalimbali kwa watumiaji wa ziwa hilo wakiwemo wavuvi na wamiliki wa boti na meli kwa sababu hutanda katika eneo kubwa na kuzuia shughuli zao.

Wanafanya nini kukabiliana nayo? Msikilize mtangazaji Herimina Mkude ambaye anatoa ufafanuzi zaidi.

Feb 28, 202206:35
Simulizi ya Mtaa unaomezwa na maji ya Ziwa Victoria

Simulizi ya Mtaa unaomezwa na maji ya Ziwa Victoria

Ni Mtaa wa Ziwa mkoani Mwanza ambao umeharibiwa huku nyumba za wakazi wake zikizama kwenye maji baada ya kina cha maji cha Ziwa Victoria. 

Kuongeza kwa kina cha maji cha ziwa hilo ni matokeo ya uchafuzi wa mazingira, mafuriko na mvua kubwa iliyonyesha mwaka 2020. Wadau wa mazingira washauri watu kuondoka katika mtaa huo huku wakihimiza watu kuacha kujenga au kufanya shughuli za kilimo na uzalishaji ndani ya mita 60 ya vyanzo vya maji ili kuepuka madhara. 

Kufahamu zaidi, sikiliza makala haya yanayoleta kwenu na Herimina Mkude. 

Feb 25, 202206:57
Mashaka ya maumbile yanavyozuia penzi la kweli

Mashaka ya maumbile yanavyozuia penzi la kweli

Kwa maringo na mikogo ya Roxanne, unaweza kuhisi ni wa kishua au ana kila kitu lakini huwezi amini, na urembo wake wote alionao, anadaiwa kodi ya pango na kila siku anakimbizana na mwenye nyumba.

Feb 18, 202208:48
Filamu ya Brazen: Maandishi yanayomuwinda mwandishi wa vitabu

Filamu ya Brazen: Maandishi yanayomuwinda mwandishi wa vitabu

Filamu ya “Brazen” inamuhusu mwanamama Grace Miller ambaye ni nyota maarufu wa vitabu vya simulizi nchini Marekani ambaye maandishi yake yanaanza kugeuka uhaisiana kumuwinda.

Feb 11, 202207:06
Kifahamu kisa cha kuumiza kinachoihusu kampuni ya Gucci

Kifahamu kisa cha kuumiza kinachoihusu kampuni ya Gucci

Patrizia anavutiwa na kijana mmoja anaekutana naye kwenye party hiyo.

Unaweza kuelezea hisia alizo nazo kama mtu kupata msamaha wa deni la timiza au kuwa zamu katika kupokea hela ya kikoba. Bila shaka unajua hisia hizo.

Feb 04, 202208:14
Filamu: Dunia inampatia mwanamfalme nafasi ya kuchagua kati ya nchi yake na huba.

Filamu: Dunia inampatia mwanamfalme nafasi ya kuchagua kati ya nchi yake na huba.

Izzy anajikuta akivunja kibubu chake alichojitunzia kwa muda mrefu kwa ajili ya kusafiri sehemu mbalimbali duniani.

Jan 28, 202207:12
Utafanya nini pale ndoto yako inapokuingiza matatani?

Utafanya nini pale ndoto yako inapokuingiza matatani?

Siku moja Bom akiwa katika shughuli za kikazi, anaona wafanyakazi wenzie wawili  wanapigana, lakini anaposogea kwa karibu anakutana na kitu tofauti.

Mfanyakazi mmoja ametapakaa damu usoni na anapomtazama kwa karibu anagundua kuwa mtu huyo amebadilika na kuwa kama ‘Zombie’.

Jan 21, 202208:42
Ifahamu filamu ‘inayotrend’ kwenye mitandao ya Kijamii Tanzania

Ifahamu filamu ‘inayotrend’ kwenye mitandao ya Kijamii Tanzania

Changamoto za mahusiano, malezi, umaskini na mategemeo zote zimeelezewa kupitia wahusika wanne: Tumaini, Angel, Stella pamoja na Rose.

Jan 14, 202209:26
Safari ya ndugu waliopotezana kutafuta ukweli wa wazazi wao

Safari ya ndugu waliopotezana kutafuta ukweli wa wazazi wao

Filamu hii inawahusu mabinti watano ambao kwa mara ya kwanza wanakutana katika moja ya hoteli iliyopo Cancun mjini Mexico.

Jan 07, 202209:17
Kumpoteza mtu umpendaye ni mwanzo wa safari mpya

Kumpoteza mtu umpendaye ni mwanzo wa safari mpya

Filamu hii inamleta tena Buster Moon, mdau wa sanaa za maonyesho ambaye kutengeneza show ya muziki inayoweza kukusanya sayari zote ni kitu kidogo sana.

Dec 31, 202108:13
A Naija christmas : Filamu ya kuchangamsha siku kuu yako.

A Naija christmas : Filamu ya kuchangamsha siku kuu yako.

Filamu hii inahusu familia ya Madam Agatha, singo mother mwenye vijana wa kiume watatu Chike, Obi, na Ugo.

Dec 24, 202107:06
 Filamu ya king’s affection: Majukumu yanavyobadilisha jinsia

Filamu ya king’s affection: Majukumu yanavyobadilisha jinsia

Filamu hii inaturudisha nyuma enzi hizo wakati nchi ya Joeson haijaitwa Korea. Katika kipindi hicho, Mwana mfalme mteule au “crown prince” Anatarajia mtoto ambaye atakuja kurithi kiti cha enzi kama mfalme wa Joeson.

Dec 17, 202106:18
Itakuwaje ikiwepo sayari ya wanaume peke yao?

Itakuwaje ikiwepo sayari ya wanaume peke yao?

Ni filamu inayomhusu mwanadada ambaye anajikuta katika sayari iliyo na wanaume tu baada ya kupata ajali.

Dec 10, 202104:47
Huyu ndiye mwanamke shujaa wa Afrika

Huyu ndiye mwanamke shujaa wa Afrika

Historia ya malkia huyu inatufanya turudi nyuma miaka 500 iliyopita, ambapo Amina akiwa ni ‘princess’ mdogo mwenye ujasiri na kipenzi cha baba yake.

Nov 29, 202105:42
Filamu ya ‘Red Notice’: Kikulacho ki nguoni mwako

Filamu ya ‘Red Notice’: Kikulacho ki nguoni mwako

Filamu ya “Red Notice”, ipo kutukumbusha kuwa makini na wale wageni wanaogonga kwenye milango ya mioyo yetu na kutufanya tuone kuwa dhamira zao juu yetu ni za dhati.

Nov 19, 202107:00
Filamu ya “No Time To Die”: Mashaka yaliyojaa majuto

Filamu ya “No Time To Die”: Mashaka yaliyojaa majuto

Bahati ya mapenzi siyo ya wote, Wakati Adamu akikutana na Hawa kwa urahisi, wengine ni Samson wanaoishia na Delila. Samson wa leo ni James Bond almaarufu kama Agent 007.

Nov 12, 202106:02
Pesa zilivyoweka rehani maisha ya vijana watano

Pesa zilivyoweka rehani maisha ya vijana watano

Ni katika filamu ya Filamu ya the Army of Thieves inayohusu kikundi cha wezi waliobobea kuibia mabilionea

Nov 05, 202105:20
“My Name” Filamu ya kuchangamsha wikiendi yako

“My Name” Filamu ya kuchangamsha wikiendi yako

Katika filamu hii  ya “My name”, yaani jina langu, tunakutana na binti mrembo Yoo Ji Woo, ambaye katika maisha yake amekuwa akilelelewa na baba yake tu.

Kwa jinsi baba yake alivyokuwa akimpenda sana, basi Jiwoo anaweza kujiita “dad’s daughter” kama vile wadada huwa wanajigamba.

Maisha ya Jiwoo na baba yake siyo mazuri sana, kwani baba yake hakuwa na kazi rasmi ya kuwaingizia kipato zaidi ya kuwa mtu tuanayejihusisha na kazi haramu au tunaweza kumuita ‘gangstar’

Licha ya umaskini wao, maisha ya upendo na  furaha yalikuwa ni kila kitu.

Maisha ya Jiwoo yanakuja kubadilika siku ambayo anatimiza miaka 17, kwani siku hiyo baba yake anaaga dunia kwa kupigwa risasi tena mbele ya macho yake.

itakuaje? Ji Woo atalipiza kisasi na kumsaka muuaji wa baba yake? Fuatili simulizi hii mpaka mwisho.

Oct 22, 202106:30
Mfahamu ‘single mother’ mpambanaji wa filamu ya Maid

Mfahamu ‘single mother’ mpambanaji wa filamu ya Maid

Clean Bandit hawakukosea walipoimba kibao Cha Rockabye, ambacho kinaelezea jinsi single mothers wengi wanavyopambana kwa hali na mali ili kuwalea watoto wao.

Oct 15, 202106:26
Wanawake na safari ya ushiriki maendeleo Kigoma

Wanawake na safari ya ushiriki maendeleo Kigoma

Ushiriki wa wanawake katika maendeleo ya kata zao umechangia kuwepo kwa huduma muhimu za kijamii ikiwemo shule.

Oct 13, 202104:16
Wema unaosukuma maendeleo ya elimu Tanzania

Wema unaosukuma maendeleo ya elimu Tanzania

Kutana na watu wanaochangia maendeleo ya elimu Mkoani Kigoma kwa kuwasaidia wanafunzi kuvuka mto ambao umekuwa kikwazo cha elimu Mkoani humo.

Oct 13, 202103:50
Maisha ya ahueni baada ya Teleza

Maisha ya ahueni baada ya Teleza

Teleza ni wahalifu waliokuwa wanajipaka mafuta mwilini au oili na kuwabaka wakina mama mkoani kigoma. 

Oct 12, 202103:56
Matumaini mapya baada ya ujenzi wa shule kukwama Kigoma

Matumaini mapya baada ya ujenzi wa shule kukwama Kigoma

Endapo serikali itachelewa kukamilisha mradi wa shule hii, huenda ikachangia kwa wananchi kukata tamaa ya kujitoa kwenye shughuli za maendeleo.

Oct 12, 202103:30
Utafanya nini iwapo hakuna anayekuamini tena?

Utafanya nini iwapo hakuna anayekuamini tena?

Ni filamu ya “The Last Duel”, inayohusu kufa kwa uaminifu kati ya Marguerite na watu wake wa karibu

Oct 08, 202106:37
Filamu ya The Squid Game: Tamaa mbele mauti nyuma

Filamu ya The Squid Game: Tamaa mbele mauti nyuma

Uchambuzi wa filamu ya ‘The Squid Game’ inakukutanisha na watu wanaofanya maamuzi magumu baada ya maisha yao kutokuwa na ahueni kila uchao, huku mmoja wapo akiwa ni Gi-Hun.

Hun ni mhusika mkuu katika filamu hii, ambaye maisha yake amekuwa akiyaendesha kwa ‘kuunga unga’ tu, huku kazi yake kubwa ikiwa ni kucheza kamali.

Oct 01, 202104:55
Saa 24 za kummaliza rafiki aliyegeuka kuwa adui

Saa 24 za kummaliza rafiki aliyegeuka kuwa adui

Filamu ya Kate inamhusu mwanadada ambaye hajawahi kufaidi mapenzi ya baba na mama, kwani waliomleta duniani walifariki akiwa bado ni mtoto.

Sep 24, 202108:07