Naweza Show
By Naweza Show
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza.
Sikiliza kipindi cha Naweza
| Radio Free Afrika kila Jumamosi saa 11 jioni
| Radio TBC Taifa kila Jumapili saa 11:30 jioni
| Radio One kila Jumamosi saa 2:15 usiku
Kipindi cha Naweza Show kinaletwa kwenu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma (HPS)
Naweza ShowMar 26, 2019
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 10:Umuhimu wa Afya ya Uzazi kabla na baada ya ujauzito
Hapa tunakuletea simulizi kutoka kwa Salome. Binti huyu alikuwa na ndoto ya kuwa fundi cherehani lakini aliozeshwa na familia akajikuta akipata mtoto na ndoto kupotea ilionekana kama ndoto yake ilikuwa matatani lakini baadae Salome alifanikiwa, Je alifanyaje?
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 9: Umuhimu wa kumnyonysha mtoto maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo bila kumpa kitu chochote..
inakuletea simulizi kutoka kwa Chagu. Mama mkwe wake na Chagu hakuona umuhimu wa Chagu kumnyonyesha mwanae mchanga maziwa yake tu kwa miezi sita ya mwanzo, ni yapi yalimsibu chagu baada ya hapo.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 8: Umuhimu wa kumpeleka mwanao katika kituo cha kutolea huduma za afya ili apate chanjo na kujenga kinga ya mwili wake.
Hapa tutasikiliza simulizi ya Maua na mumewe Kingolile hawa wawili hakukamilisha ratiba za chanjo ya mtoto wao hivyo ikawapelekea kumuuguza kwa mda mrefu.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 7: Hatua za kuchukua pale tunapoona Dalili za Hatari kwa Mtoto Mchanga na jinsi ya kumkinga dhidi ya magonjwa.
Sehemu ya 7 ya Naweza Show inakuletea simulizi kutoka kwa Tulia. Yeye ni binti aliyepitia maisha mengi magumu na machungu ndani ya jiji la dar es salaam, na tunajifunza umuhimu wa kuwapeleka watoto wetu katika vituo vya kutolea huduma za afya pale tupoona dalili hatarishi kwao na tunashauriwa kutowapa dawa watoto wetu bila kuwapima na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 6: Umuhimu wa Kumnyonyesha mtoto mchanga maziwa ya mama pekee kwa muda wa miezi sita ya awali.
Sehemu ya 6 ya Naweza Show inakuletea simulizi kutoka Mama kiko.
Yeye ni Mama ila alishindwa kabisa kufuata kanuni za kumnyonyesha mwanae kwa kipindi cha miezi sita, sasa ni yapi yalimsibu mama kiko baada ya hapo? Simulizi hii itakufunza umuhimu ya maziwa ya mama kwa mtoto ndani ya miezi sita ya mwanzo bila kumpatia kitu chochote kile zaidi ya maziwa ya mama.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 5: Umuhimu wa Afya ya Uzazi kabla na baada ya ujauzito
Katika sehemu ya pili ya msimu mpya wa Naweza Show tunasikiliza simulizi kutoka kwa Bupe.
Simulizi hii itakufunza mengi kuhusu umuhimu wa afya ya uzazi kabla na baada ya ujauzito.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 4: Hatua za kuchukua pale tunapoona Dalili za Hatari kwa Mtoto Mchanga na jinsi ya kumkinga dhidi ya malaria.
Katika sehemu ya nne ya msimu mpya wa Naweza Show tunasikiliza simulizi kutoka kwa Sitti.
Simulizi hii itafundisha mengi kuhusu hatua za kuchukua pale tunapoona dalili za hatari kwa mtoto. Na jinsi gani wanaume wanapaswa kushiriki katika malezi ya watoto na kuwapeleka watoto katika vituo vya kutolea huduma za afya pale tu waonapo dalili za hatari.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 3: Hatua za kuchukua pale tunapoona Dalili za Hatari kwa Mtoto Mchanga
Katika sehemu ya pili ya msimu mpya wa Naweza Show tunasikiliza simulizi kutoka kwa Waridi.
Simulizi hii itafundisha mengi kuhusu hatua za kuchukua pale tunapoona dalili za hatari kwa mtoto mchanga.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 2: Umuhimu wa Afya ya Uzazi kabla na baada ya ujauzito
Katika sehemu ya pili ya msimu mpya wa Naweza Show tunasikiliza simulizi kutoka kwa Bhoke.
Simulizi hii itakufunza mengi kuhusu umuhimu wa afya ya uzazi kabla na baada ya ujauzito.
Naweza Show - Msimu wa 2, Sehemu ya 1: Kumpeleka mtoto kwenye kituo cha afya anapoonesha dalili ya #Malaria. #Naweza
Sikiliza simulizi ya Ruta, kutoka Bukoba. Leo tutajifunza kuhusu umuhimu wa kumuwahisha mtoto kwenye kituo cha afya pale anapoonesha dalili za #Malaria. #Naweza
NAWEZA Show - Sehemu ya 12 (Janet): Umuhimu wa mwenzi kupimwa VVU iwapo mama mjamzito anaishi na VVU
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya kumi na moja ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Janet.
NAWEZA Show - Sehemu ya 11 (Aisha): Dalili hatarishi kwa mtoto
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya kumi na moja ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Aisha.
NAWEZA Show - Sehemu ya 10 (Riziki): Umuhimu wa mama kujua hali yake ya afya baada ya kujifungua
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya kumi ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Riziki.
NAWEZA Show - Sehemu ya 9 (Mama Salma): Umuhimu wa kulala kwenye chandarua chenye dawa
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya tisa ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Mama Salma.
NAWEZA Show - Sehemu ya 8 (Mama Imani): Umuhimu wa kutumia uzazi wa mpango
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya nane ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Mama Imani
NAWEZA Show - Sehemu ya 7 (Samia: Umuhimu wa Kumnyonyesha mtoto mchanga maziwa ya mama ndani ya saa moja baada ya kujifungua)
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya saba ya kipindi cha Naweza, leo tena sikiliza stori ya Samia. Kupitia simulizi yake tutajifunza umuhimu wa kumnyonyesha mtoto mchanga maziwa ya mama ndani ya saa moja baada ya kujifungua.
Naweza Show - Sehemu ya 6 (Anitha - ya pili): Huduma ya Nesi kwa Mama Mjamzito aliyekuwa kwenye hali mbaya
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya sita ya kipindi cha Naweza, leo tena sikiliza stori ya Anitha. Atasimulia jinsi alivyompokea mama mjamzito aliyekuwa kwenye hali mbaya sana.
NAWEZA Show - Sehemu ya 5 (Anitha): Msaada wa Nesi kwa mama mjamzito
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya tano ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Anitha.
NAWEZA Show - Sehemu ya 4 (Mama Tabitha): Umuhimu wa kutumia dawa za ARV wakati wa ujauzito iwapo mama anaishi na VVU
Stori za Kweli, Watu wa Ukweli, Maamuzi Sahihi!
Maisha bora huanza kwa kusema #Naweza. Sikiliza sehemu ya nne ya kipindi cha Naweza, leo sikiliza stori ya Mama Tabitha
NAWEZA Show - Sehemu ya 3 (Mwajuma): Umuhimu wa mama mjamzito kutumia dawa ya SP
Sikiliza sehemu ya tatu ya show ya #Naweza.
Leo tunasikia stori ya Mwajuma inayohusu umuhimu wa mama mjamzito kutumia dawa ya SP.
NAWEZA Show Sehemu ya Pili (Sada): Ushirikiano baina ya wenzi kipindi cha ujauzito
Sikiliza sehemu ya pili ya show ya #Naweza.
NAWEZA Show Sehemu ya Pili (Sada): Ushirikiano baina ya wenzi kipindi cha ujauzito
Naweza Show Sehemu ya 1 (Mwanja): Changamoto kipindi cha ujauzito
Sikiliza sehemu ya kwanza ya show ya #Naweza.